Sunday 22 March 2015

KITABU; Jinsi Ya Kufaidika Na Mabadiliko Yanayotokea Kwenye Maisha.

Kama kuna kitu kimoja ambacho tuna uhakika nacho hapa duniani ni kwamba dunia inabadilika kila siku. Ukiangalia historia ya dunia tulikotoka na tulipo sasa kumetokea mabadiliko makubwa sana. Zilianza zama za mawe, zikaja zama za chuma, yakaja mapinduzi ya viwanda na hata sasa tupo kwenye mapinduzi ya kiteknolojia.
Jambo moja la kushangaza ni kwamba pamoja na mabadiliko haya kuwa wazi bado watu wengi ni wagumu sana kubadilika. Watu hawapendi mabadiliko, wanapenda kufanya kile walichozoea kufanya na wanataka maisha yaendelee vile yalivyokuwa jana na leo. Kitu ambacho ni ndoto isiyowezekana.
Katika zama zote ambazo dunia imepita, kuna watu ambao waliweza kubadilika haraka na kupata faida ya mabadiliko, wengine walilazimishwa kubadilika na hivyo kuburuzwa na kuna ambao waliachwa na mabadiliko na hivyo kupotea. Waliofaidika na mabadiliko ni wale waliokuwa tayari kubadilika, walioburuzwa na mabadiliko ni wale ambao walikuwa hawajui kama kuna mabadiliko ila wanakwenda tu na hali ilivyo. Walioachwa na mabadiliko ni wale ambao hata baada ya kuona mabadiliko wao waligoma kubadilika, waliendelea kung’ang’ania kile walichozoea na hatimaye kuachwa nyuma na kupotea.
mabadiliko cover EDWEB
Mabadiliko ni jambo muhimu sana lakini watu wengi hawajalipa msisitizo kwenye maisha na hii inapelekea wengi kuachwa nyuma na mabadiliko haya.
Ni kutokana na umuhimu wa jambo hili nimekuandalia kitabu kinachoitwa JINSI YA KUFAIDIKA NA MABADILIKO YANAYOTOKEA KWENYE MAISHA.
Katika kitabu hiki utajifunza mambo yafuatayo;
1. Historia fupi ya mabadiliko kwenye maisha ya mwanadamu hapa duniani na kwa nini mabadiliko yataendelea kutokea.
2. Mabadiliko makubwa yanayotokea kwenye elimu, kazi na hata biashara.
3. Makundi ya aina tatu ya watu ambao wanazalishwa na mabadiliko, kundi linalonufaika na mengine yanayopoteza.
4. Mambo kumi muhimu sana ya kufanya ili na wewe uingie kwenye kundi ambalo linanufaika sana na mabadiliko ambayo yanaendelea kutokea
5. Mabadiliko makubwa yanayokuja kwenye mfumo wa elimu, mfumo wa ajira na hata biashara na ujasiriamali.
Kitabu hiki kitakuandaa wewe na kukupa mbinu za kuweza kuboresha maisha yako zaidi na kufanikiwa licha ya mabadiliko yanayoendelea.
Kitabu hiki ni muhimu sana kwa makundi yafuatayo;
1. Wanafunzi wa vyuo vikuu ambao wanasoma ila hawana uhakika wa kupata ajira. Kitawawezesha kujiandaa mapema ili kujua njia watakayochukua na hivyo kutopoteza muda wakisubiri ajira ambazo hazipo.
2. Wafanyakazi ambao wamekuwa kwenye kazi kwa muda mrefu lakini hawaoni manufaa ya kazi zao kwenye maisha yao.
3. Wafanyabiashara ambao wamefanya biashara kwa muda mrefu ila wako pale pale miaka nenda miaka rudi.
4. Wafanyakazi ambao wamestaafu kazi, wamefukuzwa kazi, wamepunguzwa kazi au wameamua kuacha kazi wenyewe.
5. Watu ambao umri wao umekwenda kiasi na wanaamini kwamba mambo waliyokuwa wanafanya zamani ni bora kuliko yanayofanyika sasa, na wanaendelea kuyafanya licha ya kushindwa kupata majibu makubwa.
6. Mtu yeyote ambaye anataka kuboresha maisha yake zaidi, kwa kujua mambo yanayoendelea na ni yapi yanakuja kwa siku za mbeleni.
Ni muhimu sana wewe kupata na kusoma kitabu hiki, kitaleta mabadiliko makubwa sana kwenye maisha yako kama utakuwa tayari kufanyia kazi yale ambayo utajifunza.
JINSI YA KUPATA KITABUJINSI YA KUFAIDIKA NA MABADILIKO YANAYOTOKEA KWENYE MAISHA.
Kitabu hiki kipo kwenye mfumo wa soft copy yaani pdf na unaweza kukisoma kwenye simu yako kama ni smartphone, unaweza kukisoma kwenye tablet na pia unaweza kukisoma kwenye kompyuta. Kurasa zake zinasomeka vizuri kwenye vifaa hivyo vya aina tatu tofauti.
Gharama ya kitabu hiki ni tsh elfu tano(5,000/=), gharama hii ndogo sio kwa sababu kina mambo madogo ila ni kwa sababu kitabu hiki ni muhimu sana na kila mtu ni muhimu akisome, hivyo gharamaisiwe kikwazo cha watu kushindwa kukisoma.
Kupata kitabu unafanya malipo ya tsh 5,000/= kupitia namba 0717396253 au 0755953887 na kisha unatuma email yako kwenye moja ya namba hizo na unatumiwa kitabu mara moja.
Mambo sasa hivi yanakwenda kidigitali zaidi na huna haja ya kubeba mizigo mingi, kwa kuwa na simu yako tu unaweza kuendelea kujifunza mambo mengi sana.
Karibu sana upate kitabu hiki mapema, kwa sababu jinsi unavyozidi kuchelewa kukipata, mabadiliko yanaendelea kutokea na yanakuacha nyuma. Jinsi utakavyoweza kuchukua hatua haraka ndivyo unavyoweza kuiokoa na kuimarisha kazi yako au biashara yako. Chukua hatua haraka kwa kusoma kitabu hiki leo.
Pia tembelea blog ya VITABU VYA UJASIRIAMALI NA MAFANIKIO ili kupata vitabu vingine vingi na vizuri vya kukuwezesha kufikia mafanikio makubwa kwenye jambo lolote unalofanya.
Jipatie kitabu chako leo, maisha hayakusubiri wewe uwe tayari.
Nakutakia kila la kheri katika safari yako ya kuboresha maisha yako, na kitabu hiki kiwe nguzo muhimu sana kwako.
TUPO PAMOJA.
MAKIRITA AMANI
makirita@kisimachamaarifa.co.tz

KITABU; Jinsi Ya Kutengeneza Fedha Kwenye Mtandao Kwa Kutumia Blog.

Wiki chache zilizopita AMKA MTANZANIA iliendesha mafunzo mafupi ya jinsi ya kutengeneza fedha kwenye mtandao kwa kutumia blog. Mafunzo haya yalikuwa na mafanikio makubwa sana kwani washiriki walijifunza mbinu mbalimbali za kuweza kukuza blog zao na kuzibadilisha kuwa biashara.
Pamoja na kutoa muda mrefu wa kujiunga na mafunzo haya, bado kuna watu wengi sana ambao waliyakosa mafunzo haya. Baada ya mafunzo kuisha kila siku kumekuwa na watu ambao wanahitaji kupata mafunzo haya. Ni vigumu kurudia kuendesha tena mafunzo haya kwa sababu kuna vitu vingi vya kufanya wakati wa kuendesha mafunzo ndio maana kuna ratiba maalumu za kuendesha mafunzo.
Kwa kuwa elimu hii ni muhimu sana na inaweza kumkomboa mtanzania yeyote anayetaka kutengeneza kipato kikubwa nimeona sio busara kwa watu wengi kuikosa elimu hii. Hivyo nimetoa kitabu kinachoitwa JINSI YA KUTENGENEZA PESA KWENYE MTANDAO KWA KUTUMIA BLOG. Kitabu hiki kimejaa mbinu muhimu za kutengeneza fedha ambazo ainafanya kazi kwenye mazingira yetu ya kitanzania na ndio huwa nazitumia kila siku.
Katika kitabu hiki utajifunza jinsi ya kutengeneza blog hata kama hujui kabisa na jinsi ya kuikuza na kuifanya kuwa biashara kubwa.
Kitabu hiki kina mafunzo yafuatayo;
1. Utambulisho wa blog na aina mbalimbali za blog.
2. Jinsi ya kutengeneza blog
3. Njia mbalimbali za kutengeneza fedha kupitia blog.
4. Kuweka misingi ya blog yako na kuchagua mtindo wako.
5. Uandishi wa makala zenye mvuto.
6. Kujenga hadhira na kuvutia wasomaji wengi zaidi(email list).
7. Kuunganisha blog na mitandao mingine ya kijamii ili kupata wasomaji wengi zaidi.
8. Kuchagua njia ya kuingiza fedha kutumia blog.
9. Uandishi wa makala za kuuzia bidhaa au huduma na siri iliyoko nyuma ya utafutaji wa masoko.
10. Kutengeneza fedha kusiko na kikomo kupitia blog yako.
11. Kutofautisha blog yako na blog nyingine na jinsi ya kuendelea kuikuza zaidi.
Masomo hayo yameelezewa kwa lugha rahisi na wakati mwingine kwa kutumia picha ili kuweza kukurahisishia wewe kuelewa.
COVER
Pata kitabu hiki mara moja ili uweze kutengeneza misingi yako ya kuweza KUTENGENEZA KIPATO KISICHO NA KIKOMO KWENYE MTANDAO KWA KUTUMIA BLOG.
Kitabu hiki kipo kwenye mfumo wa PDF na kinatumwa kwa njia ya EMAIL.
Gharama ya kitabu hiki ni tsh elfu kumi(10,000/=) unatuma fedha hiyo kwa MPESA-0755953887 AU TIGO PESA-0717396253 kisha unatuma email adress yako kwa meseji kwenye moja ya namba hizo na unatumiwa kitabu mara moja.
Pata kitabu hiki na uanze kujenga misingi ya kutengeneza pesa kupitia mtandao. Uzuri wa kutengeneza pesa kwenye mtandao ni kwamba hakuna kikomo na unaweza kufanya kazi popote ulipo. Kikomo cha kiwango cha fedha unachoweza kutengeneza unaweka mwenyewe, ukiwa na juhudi na maarifa kipato kinakuwa kikubwa. Unaweza kufanyia kazi zako ofisini, nyumbani au sehemu yoyote unayoona ni nzuri kwako.
Kupitia kitabu hiki unapata nafasi kubwa ya kuyaboresha maisha yako.
Karibu sana upate kitabu hiki ambacho kitaboresha maisha yako kwa kiasi kikubwa sana.
TUKO PAMOJA.

Kitabu; Kwa Nini Mpaka Sasa Wewe Sio Tajiri.

Waswahili wanasema huwezi kutatua tatizo usilolijua. Baada ya kufuatilia kwa kina sana kuhusiana na jitihada za watu kuondoka kwenye umasikini na kuwa matajiri nimegundua kwamba wengi wetu tunajaribu kutatua tatizo tusilolijua.
  Unapojaribu kutatua tatizo usilolijua huishii tu kushindwa kutatua tatizo hilo bali unazidi kuwa kwenye hali mbaya zaidi kwa kukosa suluhisho na kuendelea kutafuta suluhisho huku ukizidi kupotea.
  Katika tatizo letu la umasikini tumekuwa tukijipa sababu nyingi sana kwa nini hatujaweza kuwa matajiri. Lakini asilimia tisini ya sababu hizo ni za uongo. Na hata hiyo asilimia kumi ambazo ni za ukweli bado hatuna suluhisho la sababu hizo.
kitabu kava
  Tunakuwa na sababu za uongo kwa sababu hakuna sehemu yoyote kwenye mfumo wa elimu tunakofundishwa jinsi ya kutengeneza utajiri. Na kwenye jamii kwa kuwa masikini ni wengi zaidi ya matajiri hakuna kikubwa tunachoweza kujifunza kutoka kwenye jamii.
  Kwa kukosa elimu hii muhimu watu tumekuwa tukienda kwa kubahatisha na kufanya majaribio mbalimbali ya kutufikisha kwenye utajiri. Kwa kutokuwa na elimu ya kutosha mengi ya majaribio tunayofanya yanazidi kutupoteza na kufanya maisha yetu kuwa magumu zaidi.
  Kwa kuona umuhimu wa elimu hii kwangu na kwa watanzania wenzangu nimeandika kitabu kinachoitwa KWA NINI MPAKA SASA WEWE SIO TAJIRI, sababu ishirini na tano zinazokuzuia wewe kufikia utajiri. Kitabu hiki kipo kwenye mfumo wa softcopy wa PDF na unaweza kukisoma kwenye kompyuta yako au simu yako kama ina uwezo wa kusoma vitabu.
kitabu kava2kitabu kava3
Kitabu hiki ni kifupi sana, kina kurasa 81, ila kimejaa mafunzo ambayo kama ukianza kuyatumia utaona mabadiliko makubwa sana kwenye maisha yako. Nimejitahidi kukifanya kitabu hiki kuwa kifupi ili hata wale ambao ni wavivu wa kusoma waweze kusoma kitabu hiki. Pamoja na kuwa kifupi, mafunzo yaliyopo ndani yake ni makubwa sana na unayahitaji sana ili uweze kutoka hapo ulipo.
  Kwenye kitabu hiki utajifunza sababu ishirini na tano kwa nini mapaka sasa wewe sio tajiri. Na pia kwenye kila sababu utajifunza ufanye nini ili uweze kuondoka kwenye umasikini na kuingia kwenye utajiri.
  Kitabu hiki kitapatikana kwa gharama ndogo sana ya shilingi za kitanzania elfu tano(5,000/=) ili kila mtanzania aweze kukisoma na kutumia mafundisho hayo kuboresha maisha yake.
  Kupata kitabu hiki tuma fedha tsh elfu tano kwa tigo pesa(0717396253) au mpesa(0755953887) na kisha tuma email yako kwenye moja ya hizo namba na utatumiwa kitabu chako. Kwa mawasiliano zaidi unaweza kutumia namba hizo au email amakirita@gmail.com
  Wahi upate kitabu hiki mapema ili uendeleze mabadiliko makubwa kwenye maisha yako.
  Nakutakia kila la kheri na tuko pamoja kwenye safari hii.